Katibu Mkuu
wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Dkt. Maasa Ole
Gabriel, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa busara na hekima zake
zilizoifanya Tanzania kuendelea kuwa salama na yenye amani
Ameipongeza
hatua ya kuanzisha mchakato wa maridhiano kupitia Tume ya kuchunguza
matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi
mkuu wa Oktoba 29, 2025.
Askofu Dkt. Maasa ametoa kauli hiyo
Aprili 3, 2026 katika ofisi za Jumuiya hiyo jijini Arusha, wakati taifa
likisubiri kupokea ripoti ya tume hiyo. Amesisitiza kuwa ni umuhimu kwa
Watanzania kuendelea kuwa watulivu na kudumisha mshikamano uliopo
nchini.
Amesema ripoti hiyo itajumuisha maoni ya makundi
mbalimbali yaliyoguswa na matukio hayo, wakiwemo vijana, viongozi wa
dini na siasa pamoja na wanajamii wengine. Ameongeza kuwa JMAT
itaendelea kusisitiza umuhimu wa kulinda tunu za taifa, ikiwemo amani,
upendo na mshikamano.
Aidha, amewahimiza wananchi kusubiri kwa
utulivu hatua zitakazochukuliwa baada ya Rais kupokea na kupitia
mapendekezo yaliyomo kwenye ripoti hiyo, akieleza kuwa umoja na amani ni
rasilimali muhimu kwa maendeleo ya taifa.
0 Comments